Kupambanua kanuni zinazotawala mageuzi katika sentensi sahili ya Ekegusii language in Kenya

https://doi.org/10.51317/ecjkisw.v4i1.364

Authors

  • Wilfrida Kemuma Mounk Kenya university, Kenya.

Keywords:

mageuzi, sentensi sahili

Abstract

Utafiti huu unalenga kupambanua kanuni zinazotawala mageuzi katika sentensi sahili ya Ekegusii language in Kenya. Nadharia ya Sintaksia Finyizi na Sarufi Geuza Maumbo uliongoza utafiti huu. Utafiti huu ulikuwa wa maktabani, kwa kutumia kifaa cha kudondoa data, vitabu teule vya Ekegusii ulitumika katika kusanya data. Mbinu ya usampulishaji kwa lengo maalum ilitumika kwa lengo la kupata sentensi ambazo hudhihirisha mageuzi. Data iliwasilishwa kwa njia za maelezo. Utafiti huu ulidhihirisha kuwa Ekegusii na sheria na kanuni zinazotawala mageuzi hayo. Mageuzi ya kisintaksia huleta mabadiliko mengi katika sentensi asili. Kanuni geuzi husababisha athari mahsusi katika sentensi kimuundo, kimofolojia na kifonetiki lakini kisemantiki sentensi huwa ni ile ile. Nadharia za Sintaksia Finyizi pamoja na nadharia Sarufi Geuza Maumbo ziliweza kuchanganua sentensi za Ekegusii kwa ukamilifu. Mapendekezo ya utafiti huu ni kufanya aina zingine za mageuzi kama vile, geuzi hamishi swalifu, geuzi hamishi la yambwa tendewa katika lugha hii na hata lugha nyinginezo ili kukuza uwanja wa kisintaksia. Kuna uhamisho unaotokea kwa lugha zingine nasiyo katika Ekegusii. Hizi pia zinaweza kufanyiwa utafiti. Nadharia zilizoongoza utafiti huu ni zile za Sintaksia Finyizi na Sarufi Geuza Maumbo. Tafiti zaidi zinaweza kufanyiwa mada hii kwa kutumia nadharia zingine ili kueleza ikiwa kutakuwa na matokeo tofauti.

Downloads

Download data is not yet available.

Published

2022-04-20

How to Cite

Kemuma, W. (2022). Kupambanua kanuni zinazotawala mageuzi katika sentensi sahili ya Ekegusii language in Kenya. Editon Consortium Journal of Kiswahili, 4(1), 440–444. https://doi.org/10.51317/ecjkisw.v4i1.364

Issue

Section

Articles