Matumizi ya Mtindo na Mbinu za Lugha katika Nyimbo za Kampeni za Urais Nchini Kenya (2002–2022)
Keywords:
Diskosi, kampeni, lugha, nyimbo, siasaAbstract
Makala hii inachunguza matumizi ya mtindo na mbinu za lugha katika nyimbo za kampeni za urais nchini Kenya kati ya mwaka 2002 na 2022. Tofauti na tafiti nyingi zilizojikita katika hotuba na mikutano ya kisiasa, utafiti huu unazingatia nyimbo za kampeni kama maandiko ya kisiasa yenye ushawishi mkubwa katika kujenga mitazamo ya wapiga kura. Nyimbo nane (8) zilichaguliwa kimaksudi kutoka chaguzi tano za urais kwa kuzingatia umaarufu, usambazaji mpana kupitia vyombo vya habari, na mchango wake katika kujenga taswira ya wagombea. Data ilikusanywa kati ya Januari na Juni 2024 na kuchambuliwa kwa kutumia uchambuzi wa maudhui kupitia mbinu ya kithamano ya kimaelezo. Matokeo yanaonyesha kuwa mbinu za lugha kama takriri, mwito-na-mwitiko, sitiari, methali, nahau, chuku, lugha ya hisia na uchanganyaji wa ndimi zilitumiwa kimkakati kuhamasisha wapiga kura na kuimarisha ujumbe wa kisiasa. Takriri na mwito-na-mwitiko zilikuza mshikamano na ushiriki wa hadhira, huku sitiari, methali na nahau zikijenga matumaini, kuhalalisha ujumbe na kuimarisha uhusiano wa kijamii. Aidha, uchanganyaji wa Kiswahili na lugha za kimaeneo uliimarisha utambulisho wa pamoja, na nyimbo zenye jazanda na lugha ya hisia zilihusishwa na ongezeko la hamasa katika mikutano ya kampeni. Utafiti unahitimisha kuwa matumizi ya lugha katika nyimbo za kampeni ni ya kimkakati na yana mchango mkubwa katika kuunda mitazamo na kuelekeza maamuzi ya kisiasa. Unapendekeza tafiti zijazo zichunguze athari za nyimbo hizi kwa makundi mbalimbali ya kijamii na kuhimiza uwajibikaji katika matumizi ya lugha ya kampeni.
Downloads
Published
How to Cite
Issue
Section
Copyright (c) 2026 Margan Adero Carlpeters, Samuel M. Obuchi, Mosol Kandagor

This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License.

