Uimarishaji wa Lugha za Kiasili Kupitia Vyombo vya Habari: Mfano wa Kinandi katika Runinga ya Kass
Keywords:
Kilimo, kinandi, lugha, runinga, wakulimaAbstract
Kiswahili
Lugha za kiasili ni muhimu sana katika kufanikisha mawasiliano kwa kuwa hutumiwa na watu wengi. Hata hivyo lugha hizi zinapitia changamoto kwa kuwa idadi ya wazungumzaji inazidi kupunguka. Hii ni kwa sababu lugha hizi zinapuuzwa huku lugha za Kiswahili na Kingereza zikitukuzwa. Hali hii inawafanya watu wengi kutumia Kiswahili katika mawasiliano ya mara kwa mara. Kutokana na umuhimu wa lugha za kiasili, ipo haja ya kuziimarisha. Makala hii inafafanua jinsi vipindi vya kilimo katika runinga ya Kass vinachangia katika uimarishaji wa lugha ya Kinandi. Uchunguzi uliozaa makala hii ulifanyika katika kaunti ya Nandi. Uliongozwa na Nadharia ya Mawasiliano ya Sperka (1966). Washiriki 264 waliteuliwa kinasibu ili kuhusishwa katika uchunguzi. Mbinu za hojaji, utazamaji na mahojiano zilitumika katika kukusanya data. Data zilikusanywa kwa kutumia mwongozo wa utazamaji, hojaji na mwongozo wa maswali ya mahojiano. Data zilizokusanywa zilichanganuliwa kitakwimu na kimaelezo kwa kuzingatia lengo la utafiti kisha zikawasilishwa kwa kutumia asilimia na majedwali. Kutokana na uchunguzi huu, tumetambua kuwa lugha ya Kinandi inaweza kuimarishwa kupitia njia zifuatazo: Kuhimiza matumizi ya Kinandi katika mawasiliano ya mara kwa mara, kuwafundisha watoto kama lugha ya kwanza, kufundisha shuleni kama mojawapo ya masomo, kuhimiza matumizi katika vyombo vya habari na kuhifadhi kwenye maandishi.
English
Indigenous languages are important in ensuring effective communication because they are used by many people. Even though they are important, these languages are going through challenges because the number of users continues to decrease. This is because indigenous languages are being neglected, whereas the use of Kiswahili and English is promoted. With this, many people use Kiswahili frequently as a form of communication. Because of the importance of indigenous languages, there is a need for them to be strengthened. This paper explains how agricultural programs aired by Kass television contribute to the strengthening of the Nandi language. This study was done in Nandi County. It was guided by Sperka’s (1966) theory of communication. Two hundred sixty-four viewers were selected randomly and involved in data collection. Questionnaires, viewing, and interviews were used to collect data. Data collection tools used included: observation schedule, questionnaire and interview guide. The data collected was analysed using percentages and tables. Thereafter, this data was presented in line with our research objective. From the results of this study, it was realised that, Nandi language can be strengthened in several ways including; encouraging use of Nandi language frequently in communication, teaching young children as their first language, including Nandi as language to be taught in schools, encouraging its use in broadcast media and preserving it in written form.

