AMEZIDI IMEZIDI

Authors

  • Matthew Kwambai Chuo Kikuu cha Egerton, Kenya

DOI:

https://doi.org/10.51317/ecjkisw.v4i1.362

Keywords:

chuku, kithiri, muundo, ukengeushi, uwasilishaji

Abstract

Makala haya yamelenga kuangazia muundo wa kipekee wa tamthilia hii na kuona jinsi muundo huu unavyowezesha uwasilishaji wa ujumbe wake. Tamthilia ya Amezidi ina muundo ambao ni tofauti na tamthilia nyingi za Kiswahili zilizoandikwa wakati mmoja. Nadharia iliyotumiwa katika kazi hii ni ya umuundo ambao unasema kuwa kazi ya fasihi inakuwa na muundo Fulani ambao unahusisha fani ambazo zitaweza kutumika katika kuwasilisha ujumbe na hivyo maudhui huwa na uhusiano mkubwa sana na fani zitakazotumiwa kuyawasilisha. Utafiti huu ulikuwa wa kimaktaba, ambapo vitabu mbalimbali vilirejelewa huku yaliyomo katika tamthilia ya Amezidi yakihakikiwa. Matokeo yalidhihirisha kuwa Wahusika wawili na wa pekee ambao wanatekeleza majukumu yote katika tamthilia yote, mbinu kama vile uradidi na chuku zinatumiwa na wahusika hawa kuendeleza maudhui kama vile: umaskini, utegemeaji wa misaada na ndoto zisizoweza kutimizwa. Kutokana na haya yote inadhihirika kuwa tamthilia hii ya kukithiri mipaka ya uhalisia inakengeusha wahusika sawa na wasomaji wa tamthilia hii.

Downloads

Download data is not yet available.

Downloads

Published

2022-04-25

How to Cite

Kwambai, M. (2022). AMEZIDI IMEZIDI. Editon Consortium Journal of Kiswahili, 4(1), 427–433. https://doi.org/10.51317/ecjkisw.v4i1.362

Issue

Section

Articles