AMEZIDI IMEZIDI
DOI:
https://doi.org/10.51317/ecjkisw.v4i1.362Keywords:
chuku, kithiri, muundo, ukengeushi, uwasilishajiAbstract
Makala haya yamelenga kuangazia muundo wa kipekee wa tamthilia hii na kuona jinsi muundo huu unavyowezesha uwasilishaji wa ujumbe wake. Tamthilia ya Amezidi ina muundo ambao ni tofauti na tamthilia nyingi za Kiswahili zilizoandikwa wakati mmoja. Nadharia iliyotumiwa katika kazi hii ni ya umuundo ambao unasema kuwa kazi ya fasihi inakuwa na muundo Fulani ambao unahusisha fani ambazo zitaweza kutumika katika kuwasilisha ujumbe na hivyo maudhui huwa na uhusiano mkubwa sana na fani zitakazotumiwa kuyawasilisha. Utafiti huu ulikuwa wa kimaktaba, ambapo vitabu mbalimbali vilirejelewa huku yaliyomo katika tamthilia ya Amezidi yakihakikiwa. Matokeo yalidhihirisha kuwa Wahusika wawili na wa pekee ambao wanatekeleza majukumu yote katika tamthilia yote, mbinu kama vile uradidi na chuku zinatumiwa na wahusika hawa kuendeleza maudhui kama vile: umaskini, utegemeaji wa misaada na ndoto zisizoweza kutimizwa. Kutokana na haya yote inadhihirika kuwa tamthilia hii ya kukithiri mipaka ya uhalisia inakengeusha wahusika sawa na wasomaji wa tamthilia hii.